Machapisho

MBUNGE AGNES MARWA ATOA SADAKA MAALUM KUUNGA MKONO MAANDALIZI YA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHANI

Picha
Na Mwandishi Wetu, Musoma.  MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Mara, Agnes Marwa, leo ametoa sadaka maalum kwa viongozi wa dini ya Kiislamu katika Misikiti tofauti ya Musoma Mjini ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono maandalizi ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani. Sadaka hiyo imelenga kuwasaidia viongozi wa dini pamoja na waumini katika kujiandaa na mwezi huo muhimu wa ibada, unaoheshimiwa na Waislamu duniani kote. Baadhi ya vitu vilivyotolewa ni pamoja na buswati, tende, kanzu, balaghashee pamoja na fedha taslimu, ambavyo vimekabidhiwa kwa viongozi kutoka misikiti mbalimbali ya Musoma Mjini. Akizungumza wakati wa tukio hilo, Agnes Marwa alisema kuwa sadaka hiyo ni ishara ya mshikamano, upendo na heshima kwa viongozi wa dini, pamoja na kuthamini mchango wao katika kujenga maadili mema na amani ndani ya jamii. “Nimeona ni muhimu kushiriki na ndugu zetu wa Kiislamu katika maandalizi ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani. Huu ni mwezi wa ibada, subira, na kusaidiana, hivyo ni wajibu wetu kama viongozi kuende...

WATU WAWILI WASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI KWA TUHUMA ZA MAUAJI YA MWENYEKITI WA CCM TAWI LA ITUMBI MBEYA.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Mbeya.  KUPITIA mitandao ya kijamii kunasambazwa picha mjongeo akionekana mtu mmoja mwanaume ambaye anajinasibu kuhusika katika tukio la mauaji ya aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Tawi la Itumbi aitwaye Elia Richard Sambala, miaka 53, mkazi wa Itumbi Wilaya ya Chunya Mkoa wa Mbeya. Ukweli ni kwamba, Februari 11,2026 saa 7 mchana katika Kijiji cha Itumbi, Elia Richard Sambala, alikutwa shambani kwake akiwa amejeruhiwa kwa kukatwa na kitu chenye makali kichwani na watu wasiojulikana na alifariki dunia muda mfupi baada ya kufikishwa Hospitali ya Wilaya ya Chunya kwa matibabu. Kufuatia tukio hilo, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya, kupitia Askari wa kuchunguza matukio ya mauaji, walianza msako mkali na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa wawili kuhusiana na tukio hilo na ufuatiliaji zaidi kwa wengine waliohusika unaendelea. Uchunguzi wa awali umebaini kuwa, chanzo cha tukio hilo ni mgogoro wa masilahi wa eneo la uchimbaji madini ya dhahabu ambapo mmoja wa wanafamilia hao alikodi...

MATUMIZI YA KONDOMU YASHUKA KWA ASILIMIA TANO: KENGELE YA TAHADHARI KWA TAIFA

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  WAKATI  dunia ikiendelea kupaza sauti kuhusu umuhimu wa kinga dhidi ya maambukizi ya Virusi vya UKIMWI na magonjwa ya zinaa, takwimu zinaonesha kuwa matumizi ya kondomu nchini yameshuka kwa takribani asilimia tano.  Hii si namba ya kupuuzwa ni ishara inayopaswa kuamsha mjadala mpana na hatua za haraka katika kulinda afya ya jamii. Kupungua huku kunakuja licha ya kampeni za muda mrefu za uhamasishaji na upatikanaji wa kondomu katika vituo vya afya na maeneo mbalimbali ya umma.  Je, tatizo ni nini? Je, ni uchovu wa kampeni, kuongezeka kwa dhana potofu, au kupungua kwa hofu ya maambukizi kutokana na maendeleo ya tiba? Baadhi ya wananchi wa Dodoma wanasema bado kuna pengo la elimu sahihi kuhusu matumizi ya kondomu. Ingawa asilimia hiyo inaweza kuonekana ndogo kwa mtazamo wa haraka, kwa tathmini ya afya ya umma ni takwimu yenye uzito mkubwa.  Kupungua huku kunamaanisha kuwa watu zaidi wako katika hatari ya kuambukizwa au wanawake ku...

POLISI YAWASAKA "WALIOMVUTISHA" SIGARA MTOTO, KUMREKODI NA KUSAMBAZA MTANDAONI

Picha
Na Hamida Ramadhan, Dodoma.  MSEMAJI wa Jeshi la Polisi Tanzania Naibu Kamishna wa Polisi DCP David Misime leo Jumapili Februari 15, 2026  amesema Jeshi la Polisi limeanza uchunguzi na kuwafuatilia watu ambao wamesikika kwenye Kipande cha Video kilichosambaa kwenye Mitandao ya Kijamii, wakimuhamasisha mtoto mdogo wa kiume kuvuta sigara kwani kitendo hicho ni kinyume na sheria, kanuni na taratibu za kijamii. Taarifa iliyotolewa kwa Vyombo vya habari na Msemaji huyo wa Polisi imesema uchunguzi utakapokamilika hatua za kisheria zitachukuliwa, akitoa wito kwa yeyote anayewafahamu watu hao au mtoto huyo kulisaidia Jeshi la Polisi ili kuwafikia na kuokoa afya ya mtoto huyo aliyehamasishwa kuvuta sigara. "Tunatoa onyo pia kwa watu wenye tabia za kufanya vitendo vya kikatili na vya unyanyasaji kama hivyo na vinavyofanana na hivyo kwa watoto kwa lengo lolote lile." Imesema taarifa ya Polisi. Kulingana na Polisi Makao Makuu, Dodoma, wapo wanaofanya hivyo kwa watoto wadogo kwa msukumo w...

WATENDAJI SOKO LA HISA DSE WATAKIWA KUWA WABUNIFU KUVUTIA WAWEKEZAJI

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amekutana na kufanya mazungumzo na Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) Bw. Peter Nalitolela, mazungumzo yaliyofanyika leo tarehe 13 Februari 2026, Dodoma. Katika Mazungumzo hayo, Makamu wa Rais amewahimiza watendaji DSE kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kuwa wabunifu katika masuala ya masoko na kuendelea kuvutia uwekezaji. Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) Bw. Peter Nalitolela, ameahidi kuendelea kushirikiana vema na Serikali katika kutafuta mitaji ili kuweza kusaidia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 ya kufikia uchumi wa Dola za Marekani Trilioni Moja ifikapo 2050. Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) ni taasisi ya kimkakati ya Taifa inayowezesha ukusanyaji na usimamizi wa mitaji ya muda mrefu kwa ajili ya kufadhili maendeleo ya uchumi wa Tanzania. DSE ni jukwaa rasmi linalowawezesha wawekezaji wa ndani na ...

DC SENDIGA AWATAKA WACHIMBAJI KUCHANGAMKIA BIMA YA AFYA

Picha
Na Mwandishi wetu, Mirerani.  MKUU wa Mkoa wa Manyara, Queen Sendiga amewataka wachimbaji wa madini wa eneo hilo kuchangamkia bima ya afya kwa wote ili waweze kupatiwa huduma za matibabu pindi wakiugua.  RC Sendiga ameyasema hayo wakati akizungumza kwenye mkutano mkuu wa mwaka wa chama wachimbaji cha wachimbaji madini Mkoa wa Manyara MAREMA uliofanyika kwa muda wa siku mbili Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro.  Ameeleza kwamba wachimbaji madini wa mkoa huo wanatakiwa kuchangamkia fursa hiyo ya bima ya afya kwa wote. Amesema bima ya afya kwa wote unachangia shilingi 150,000 kwa mwaka na unapatiwa huduma za afya kwa kaya ya watu sita wakiwemo baba, mama na watoto wanne.  "Wachimbaji madini mnapaswa kuchangamkia hii fursa kwani unakuwa na uhakika wa kupata matibabu wewe na familia yako pindi mkihitaji huduma na hamtapungukiwa na kitu na kununiana kutaisha," amesema RC Sendiga. Ameeleza kwamba hivi sasa serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Ha...

MAREMA WAOMBA GETI LA TANZANITE KUWA WAZI SAA 24

Picha
  Na Mwandishi wetu, Mirerani.  WACHIMBAJI wa madini ya Tanzanite mji mdogo wa Mirerani wilayani Simanjiro mkoani Manyara, wameiomba serikali kuruhusu lango la kuingia na kutoka ndani ya ukuta unaozunguka migodi ya madini ya Tanzanite kuwa wazi saa 24 ili shughuli zao zifanyike vyema. Mwenyekiti wa chama cha wachimbaji madini mkoa wa Manyara, (MAREMA) Elisha Nelson Mnyawi ameyasema hayo mbele ya mkuu wa moa huo Queen Sendiga kwenye mkutano mkuu wa mwaka wa chama hicho uliofanyika mji mdogo wa Mirerani.  Mnyawi ameeleza kwamba changamoto ya lango la kuingia na kutoka ndani ya ukuta kufungwa saa 5 usiku inawakwaza wachimbaji madini ya Tanzanite. Amesema endapo lango hilo likiwa wazi saa 24 kwa siku itakuwa vyema kwani shughuli za kiuchumi zitakuwa zimeboreshwa zaidi. "Tunavipongeza vyombo vya ulinzi na usalama ndani ya ukuta kwani wanafanya kazi nzuri ila wachimbaji wangepewa fursa ya lango hilo kuwa wazi saa 24 itakuwa bora zaidi kwao," amesema Mnyawi. Amesema endapo suala...

UMIKIDO WASHIRIKI MKUTANO MKUU WA MWAKA WA VYOMBO VYA UTANGAZAJI

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  UMOJA wa Vyombo vya Habari vya Mitandao ya Kijamii Mkoa wa Dodoma (UMIKIDO) umeshiriki Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Vyombo vya Utangazaji nchini. Mkutano huo wa siku mbili unafanyika katika Ukumbi wa New Generation jijini Dodoma, ukianza leo Februari 12, 2026. Mkutano huo umeandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA). Katika mkutano huo, mada na mafunzo mbalimbali yanawasilishwa kwa waandishi wa habari pamoja na wadau wa sekta ya utangazaji.  Aidha, kunafanyika mijadala mbalimbali inayolenga kujadili masuala muhimu yanayohusu maendeleo na uboreshaji wa vyombo vya utangazaji nchini. Mkutano huo umefunguliwa rasmi na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma.

SIKU 100 ZA RAIS SAMIA ZALETA NEEMA IGUNGA

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora.  SIKU 100 baada ya kuingia madarakani katika awamu ya pili ya uongozi wake,  Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ameleta neema kwa wakazi wa Mji wa Igunga Mkoani hapa kwa kuwawezesha kupata huduma ya maji kwa masaa 24 kila siku. Akizungumza na gazeti hili jana, Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Igunga (IGUWASA) Alex Ntonge ameeleza kuwa kazi nzuri iliyofanywa na Mheshimiwa Rais imemaliza changamoto za huduma ya maji. Amebainisha kuwa maboresho makubwa ya miundombinu na kupanuliwa kwa mradi wa maji ya Ziwa Victoria kumewezesha wakazi wote wa Mji huo na maeneo jirani kupata huduma ya maji safi na salama wakati wote, kwa masaa 24 kila siku. ‘Kazi nzuri iliyofanywa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika siku 100 za kwanza tangu aingie Ofisini, imeleta neema, mabilioni aliyotuletea yameendelea kuboresha huduma ya maji na usafi wa mazingira Mji wote’, amesema. Mkurugenzi amefafanua kuwa zaidi ya asilimia 98 ya wakazi wote wa Mj...