Machapisho

WAZIRI AWESO APELEKA NEEMA URAMBO

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora. WAKAZI wa Wilaya ya Urambo Mkoani Tabora wamelipuka kwa shangwe na furaha baada ya Waziri wa Maji Jumaa Aweso kuagiza maji ya ziwa Victoria yafikishwe katika Wilaya hiyo ndani ya wiki tatu kuanzia sasa. Waziri ametoa agizo hilo jana alipokuwa akizungumza na mamia ya wakazi wa Wilaya hiyo katika Kata ya Muungano baada ya kutembelea na kukagua Mradi wa Maji wa Miji 28 unaotekelezwa na serikali ya awamu ya sita katika Wilaya tatu za Mkoa huo. Amesema kuwa serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan imetoa shilingi bilioni 143 ili kuleta maji ya uhakika ya ziwa Viktoria katika Wilaya za Kaliua, Urambo na Sikonge ambazo zinashida kubwa ya maji. ‘Mradi huu utekelezaji wake unaenda vizuri sana, ujenzi wa tanki kubwa la kupokelea maji tayari umekamilika, na nimeambiwa kuwa kipande kilichobakia hakizidi hata kilometa moja maji yatakuwa yamefika hapa Urambo’, ameeleza. ‘Nitawaongezea shilingi milioni 500 za mabomba ili kazi hii ifanyike ha...

WAANDISHI KUCHUNGUZA SHOROBA NA MABADILIKO TABIA NCHI

Picha
  Na Mwandishi wetu, Arusha. Waandishi wa habari kanda ya kaskazini na kati, wamekubaliana kuandika uchunguzi wa uvamizi njia za wanyamapori (Shoroba) na athari za mabadiliko tabia nchi nchini. Mapito mengi ya wanyama nchini ikiwepo ya Kwakuchinja yaliyopo katikati ya  hifadhi ya Taifa ya Tarangire na Manyara yanaendelea kuvamiwa na watu ajili ya shughuli za kibiaadamu na kuathiri wanyamapori kuhama na biolojia yao. Mabadiliko ya tabia nchi yanayochangiwa na uharibifu wa mazingira yameanza kusababisha kumezwa ardhi maeneo kadhaa ikiwepo eneo la pangaji mkoani Tanga na ukame maeneo mengi nchini ikiwepo ya jamii za asili na kupungua barafu mlima Kilimanjaro . Maamuzi ya kufanya uchunguzi hao yalifikiwa  katika mafunzo ya uandishi wa habari za mazingira yaliyoandaliwa na mtandao wa watetezi wa haki za binaadamu(THRDC) kwa kushirikiana na Taasisi ya waandishi wa habari ya kusaidia jamii za asili (MAIPAC) kwa udhamini wa shirika la Umoja wa Mataifa la UNESCO. Akizungumza katik...

WADAU WA BIASHARA WAELIMISHWA NAMNA YA KUPATA HAKI KUPITIA BARAZA LA USHINDANI

Picha
Na.Mwandishi Wetu- Mwanza. BARAZA  la Ushindani wa Soko (FCT)  limetoa mafunzo ya kuwajengea uwezo wafanyabiashara jijini Mwanza, yakilenga kuwaongezea uelewa kuhusu masuala ya ushindani wa soko pamoja na taratibu za kupata haki katika shughuli za kibiashara. Mafunzo hayo yaliwakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya biashara, ambapo waliipongeza Wizara ya Viwanda na Biashara chini ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa juhudi zake za kuweka mazingira bora ya biashara na uwekezaji kupitia uwepo wa chombo huru cha kusimamia na kudhibiti ushindani wa soko. Akifungua semina hiyo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Bw. Balandya Elikana, alisema kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwa wadau wa sekta ya biashara kwani yanawawezesha kuelewa kwa kina majukumu ya Baraza la Ushindani pamoja na umuhimu wa mshikamano katika utekelezaji wa sheria za ushindani. “Kupitia semina hii, wadau watapata uelewa mpana kuhusu Bara...

PROF. SHEMDOE AKUTANA NA MKURUGENZI WA BENKI YA AZANIA KUJADILI MAENEO YA USHIRIKIANO

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dodoma. WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amekutana na Mkurugenzi mtendaji Benki ya Azania Bi. Esther Mangenya na kufanya mazungumzo ya namna bora ya kushirikiana katika kuboresha utoaji wa huduma za afya msingi, elimu msingi na ujenzi wa miundombinu ya barabara pamoja miundombinu ya huduma nyinginezo za kijamii. Prof. Shemdoe alifanya mazungumzo hayo na Mkurugenzi Mtendaji huyo wa Benki ya Azania hivi karibuni ofisini kwake Jijini Dodoma, alipomtembelea kwa lengo la kujitambulisha ili kujenga mahusiano mazuri ya kiutendaji yatakayowanufaisha wananchi waliopo kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa. Katika kikao kazi hicho, Prof. Shemdoe na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Azania Bi. Esther Mangenya wamekubaliana kujenga mahusiano mazuri ili wananchi wanufaike na mchango wa Serikali na benki hiyo katika kuboresha miundombinu ya utoaji wa huduma za kijamii. Kwa kutambua mchango wa taasis...

UPENDO NA MAELEWANO VYATAJWA KUWA MSINGI WA AMANI NCHINI

Picha
  Na Hamida Ramadhani, Dar Es Salaam. ADAM Seleman, Mkazi wa Msongora Jijini Dar Es Salaam amesema tafsiri halisi ya amani ni pamoja na kuelewana na kupendana miongoni mwa Watanzania, akihimiza upendo na maelewano kama msingi wa kudumisha amani na utulivu nchini. Bw. Selemani amebainisha hayo leo Jumamosi Februari 07, 2026 wakati akizungumza na mwandishi wetu wa habari kuhusu umuhimu wa amani kwa ustawi na maendeleo, akisema familia, Jamii na Nchi yoyote inahitaji amani na utulivu ili kuweza kutimiza majukumu na wajibu walionao. "Maana halisi ya amani ni ile hali ya mtu kuwa na uhuru wa kufanya jambo ambalo linaruhusiwa Kikatiba na pia amani tafsiri yake ni upendo, tukipendana ndio amani yenyewe kuanzia ndani ya nyumba. Nawaomba sana tuendelee kushikamana na kudumisha hiki tulichonacho kwani sisi nchi yetu ni kisiwa cha amani." Amesema Bw. Selemani.

AMANI INATUPA UHURU WA KUJIENDELEZA KIUCHUMI- NIACHIENI

Picha
  Na Hamida Ramadhan, Dar Es Salaam. UWEPO wa amani katika Taifa kumetajwa kama miongoni mwa rasilimali muhimu zinazohitajika ili kufanikisha malengo na mipango ya mtu mmoja mmoja, Familia, Jamii na Taifa kwa ujumla, Wito ukitolewa kwa Watanzania kuilinda na kudumisha amani. Kauli hiyo imetolewa na Bw. Ramadhan Mohamed Niachieni, Mkazi wa Mtaa wa Mkera, Kata ya Msongora Jijini Dar Es Salaam, akisisitiza kuwa amani ndiyo yenye kuleta maendeleo nchini hivyo kila mmoja anawajibika kuilinda kwa ustawi na maendeleo yetu binafsi. "Amani ina tija sana katika nchi yetu ikiwemo maendeleo ya kila hali kutokana na uhuru wa kufanya shughuli zetu za kiuchumi. Naomba sana tuilinde ili tusiharibikiwe kama wengine na ili tupate fursa ya kuijenga nchi yetu." Amesema Bw. Niachieni. Mwananchi huyo anaungana na maelfu ya wananchi wengine ambao wamekuwa wakisisitiza kuhusu ulinzi wa amani na kuwakataa wote wenye kuhatarisha amani nchini, wakirejea athari za kiuchumi na kijamii zilizojitokeza waka...

WITO WATOLEWA, JITIHADA ZA PAMOJA UDHIBITI WA SILAHA HARAMU NCHINI

Picha
  Na Hamida Ramadhan, Dar Es Salaam. KAMATI ya udhibiti na usimamizi wa silaha  imetakiwa kujikita katika utoaji wa elimu kwa jamii kuhusu madhara ya silaha haramu ili kuhakikisha wananchi wanapata uelewa wa kutosha kuhusu matumizi ya silaha haramu. Kauli hiyo imetolewa wakati wa ufungaji wa kikao cha kwanza cha mafunzo cha kamati ya udhibiti na usimamizi wa silaha, kilichofanyika kwa siku tatu Jijini Dar Es Salaam, wajumbe wakikubaliana kuwa ikiwa elimu itatolewa na jamii ikaelewa madhara ya kusambaa kwa silaha haramu, nchi itakuwa salama. Mapema akifunga kikao hicho, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, IGP Camillus Wambura amesema wajumbe wa kamati hiyo ni watu makini na wameonesha kuwa watakuwa msaada mkubwa katika kutekeleza majukumu yao kutokana na kuwa wabobezi katika nyanja tofauti kutoka Serikalini na sekta binafsi. Kwa upande wake Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini na Mrajisi Mkuu wa Silaha DCI Ramadhan Kingai alisema wataendelea kuchukua hatua kali kwa wamiliki...

WAFANYABIASHARA KARIAKOO WAPO TAYARI KWA MFUMO WA IDRAS

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dar Es Salaam. WAFANYABIASHARA wameukubali mfumo wa Usimamizi wa Kodi za ndani (IDRAS) ,huku wakijiandaa kuupokea Jumatatu ya tarehe 9 Februari mwaka huu. Akizungumza leo 6.2.2026 jijini Dar es salaam katika mafunzo ya mfumo mpya kwa wafanyabiashara wa Kariakoo Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Kariakoo (JWK) Bw. Severin Mushi amesema wapo tayari kuanza kuutumia mfumo huo kwa ushirikiano wa karibu na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Mwenyekiti huyo amesema kupitia mafunzo ambayo wamepatiwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wanaamini mfumo utakuwa msaada kwao na kuondoa changamoto mbalimbali ambazo zilikuwepo. Amesema mafunzo hayo yamekuwa msaada mkubwa kwa wafanyabiashara kwa kuwa yameondoa hofu iliyokuwepo awali na kuwapa uelewa wa pamoja kuhusu matumizi ya mfumo huo. Bw. Mushi amesema wamejiandaa kuupokea mfumo wa IDRAS, akieleza kuwa jambo lolote jipya huwa linaogopesha kwa wanaolipokea. Amebainisha kuwa mabadiliko ya kiteknolojia hayaepukiki ka...

TANZANIA, UNITAID KUIMARISHA UZALISHAJI WA BIDHAA ZA AFYA NCHINI

Picha
Na WAF, Geneva. MGANGA Mkuu wa Serikali, Dkt. Grace Magembe,  ametumia fursa ya mkutano wa 158 wa Bodi Tendaji ya Shirika la Afya Duniani (WHO) unaoendelea jijini Geneva Uswis kwa mikutano ya pembezoni kuelezea jitihada za nchi za uimarishaji wa huduma za afya. Akiwa kwenye Mkutano huo leo Februari 06, 2026, Dkt. Magembe amekutana na Mkurugenzi wa Programu wa Unitaid, Bwana Robert Matiru ambapo katika mazungumzo yao, Dkt. Magembe amesema mikakati na juhudi zinazotekelezwa na Serikali ya Tanzania, chini ya uongozi wa Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa) ikiwemo za kuweka mazingira wezeshi kwa wazalishaji wa bidhaa za afya. "Tumetumia fursa hii kukutana na shirika hili leo kwa sababu linafanya kazi na makampuni mbalimbali duniani kwa kuyaunganisha na utaalamu, mabenki na fursa za mikopo nafuu ili kuyawezesha kuanzisha viwanda vya bidhaa za afya zenye ubora na ushindani wa kimataifa," amesema Dkt. Magembe  Kwa upande wake Mkurugenzi wa Programu wa Unitaid, Bwana Robert Matir...

WAANDISHI WATAKIWA KUANDIKA UCHUNGUZI NA UWAJIBIKAJI

Picha
  Na Mwandishi wetu, Arusha. WAANDISHI wa habari za mazingira wa Kanda ya Kaskazini na Kati, wametakiwa kuandika habari za uchunguzi ambazo zinachochea mabadiliko ya sheria na sera na kuhimiza uwajibikaji. Wakitoa mada katika mafunzo ya waandishi wa habari za mazingira, yaliyoandaliwa na Mtandao wa watetezi wa haki za binaadamu (THRDC) kwa kushirikiana na Taasisi ya Wanahabari inayosaidia jamii za asili (MAIPAC), Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za waandishi wa habari nchini(UTPC), Kenneth Simbaya na Mkurugenzi wa MAIPAC, Mussa Juma wamesema wakati wa kuandika habari za matukio umepita. Simbaya amesema katika uandishi wa kisasa ni muhimu sana, habari ichochee mabadiliko ya sera na sheria badala ya kuandika matukio ya kila siku. "LHRC na MAIPAC wameandaa mafunzo haya, ili muandike habari za uchunguzi za mazingira ambazo zinachochea mabadiliko lakini pia mzingatie maadili," amesema Simbaya. Kwa Upande wake Juma, licha ya kuhimiza habari za uchunguzi ambazo zinaleta uwajibikaji kati...

WITO WA KUCHUKUA HATI KWA WATANZANIA

Picha
 

KIFO CHA MUNDE TAMBWE CHAUMIZA WENGI

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora. ALIYEKUWA Mbunge wa Viti Maalumu kupitia Chama Cha Mapinduzi kwa miaka 15, Munde Tambwe amezikwa jana katika makaburi ya Shehe Yahaya, Kata ya Ng’ambo Mjini Tabora na kuhitimisha safari yake hapa duniani. Msiba huo umevuta hisia za watu wengi wakiwemo vijana, akinamama, wana CCM, jamii, wabunge na Viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali, kutokana na ushirikiano wake mzuri, ukarimu na kujitoa zaidi kwa jamii enzi za uhai wake. Akiongea kwa niaba ya Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye msiba huo, Makamu wa Rais Dkt Emanuel Nchimbi ameeleza kuwa marehemu alikuwa rafiki wa kila mtu. Ameongeza kuwa alikuwa mtu mwema kwa jamii, wanaCCM, wabunge na viongozi wenzake na katika nafasi zote azizowahi kutumikia alitanguliza maslahi ya nchi na chama chake, hakuwa na makuu. ‘Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ametoa pole nyingi kwa wanafamilia, jamii, wabunge na wanaCCM wote kwa kuondokewa na mtu muhimu na Kada mwaminifu kwa ch...

WAANDISHI WA HABARI 140 KUJENGEWA UWEZO

Picha
  Na Mwandishi wetu, Arusha. WAANDISHI wa habari 140 wa Tanzania watajengewa uwezo wa kuandika habari za mazingira kupitia kanda mbalimbali nchini. Mkurugenzi wa shirika la waandishi wa habari la kusaidia jamii za asili (MAIPAC) Mussa Juma ameeleza kwamba waandishi hao watajengewa uwezo kupitia mtandao wa watetezi wa haki za binadamu (THRDC) kwa uwezeshaji wa shirika la umoja wa mataifa UNESCO. Mussa amesema awali wameanza kutoa mafunzo hayo jijini Arusha kwa waandishi wa habari wa mikoa ya kanda ya Kaskazini na kanda ya kati. Amesema waandishi wa habari wa mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Tanga, Manyara, Singida na Dodoma wamepatiwa mafunzo hayo  "Waandishi 140 watajengewa uwezo kwani baada ya kanda ya kaskazini, watafuata waandishi wa kanda ya ziwa, pwani na Zanzibar," amesema Mussa. Amesema waandishi hao watajengewa uwezo wa kuandika habari mbalimbali ikiwemo mabadiliko ya tabia nchi, athari za mazingira katika migodi na uchafuzi wa mazingira kwenye bahari," amesema Muss...

MAKAMU WA RAIS BALOZI DKT. NCHIMBI AMWAKILISHA RAIS. DKT. SAMIA KWENYE MAZISHI YA MBUNGE WA VITI MAALUMU TABORA MUNDE TAMBWE.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Tabora. MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM na Mbunge wa Viti Maalum Mstaafu, Marehemu Munde Tambwe, yaliyofanyika Mkoani Tabora, leo tarehe 04 Februari 2026. Akitoa salamu za rambirambi katika msiba huo, Makamu wa Rais amesema Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa salamu za pole kufuatia msiba huo mkubwa. Amesema mchango wa Marehemu Munde Tambwe ni wa kipekee sana ndani ya Taifa pamoja na Chama Cha Mapinduzi. Makamu wa Rais amesema marehemu Munde aliweka mbele maendeleo ya nchi na Chama Cha Mapinduzi na wakati wote alikuwa rafiki wa kila mtu alijali sana uhusiano mzuri. Ameongeza kwamba kufuatia marehemu Munde kuanzisha ujenzi wa msikiti ambao utahitaji ukamilishaji, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amechangia kiasi cha shilingi milioni 30 zitakaz...

POLISI MWANZA YAKANUSHA TAARIFA ZA UWEPO WA VIKUNDI VYA KIHALIFU NA UASI

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Mwanza. JESHI la Polisi Mkoa wa Mwanza limetoa wito kwa wananchi kupuuza taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii zenye kichwa cha habari kinachoeleza kuwa “kundi la uasi laibuka Mwanza, Polisi waonekana mitaani.” Kulingana na Taarifa ya Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP), Wilbrod Mutafungwa amesema taarifa hizo ni za upotoshaji zikiwa na lengo la kuleta taharuki kwa jamii, kwani wahalifu wa matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii wamekuwa wakichukua picha za askari na vitendea kazi vyao kisha kutengeneza maudhui yenye lengo la kuzua taharuki, kuchonganisha na kupandikiza chuki.  "Jeshi la Polisi linawasisitiza wananchi kuendelea kuwapuuza watu kama hao wanaosambaza taarifa zenye nia ovu na badala yake wafuatilie na kupata taarifa zenye ukweli na usahihi kutoka kwenye mamlaka zenye jukumu la kufanya hivyo." Amesema Kamanda Mutafungwa. Aidha, Jeshi la Polisi limesema linaendelea kuwafuatilia kwa karibu watu wo...