PROF. SHEMDOE AKUTANA NA MKURUGENZI WA BENKI YA AZANIA KUJADILI MAENEO YA USHIRIKIANO
Na Mwandishi Wetu, Dodoma. WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amekutana na Mkurugenzi mtendaji Benki ya Azania Bi. Esther Mangenya na kufanya mazungumzo ya namna bora ya kushirikiana katika kuboresha utoaji wa huduma za afya msingi, elimu msingi na ujenzi wa miundombinu ya barabara pamoja miundombinu ya huduma nyinginezo za kijamii. Prof. Shemdoe alifanya mazungumzo hayo na Mkurugenzi Mtendaji huyo wa Benki ya Azania hivi karibuni ofisini kwake Jijini Dodoma, alipomtembelea kwa lengo la kujitambulisha ili kujenga mahusiano mazuri ya kiutendaji yatakayowanufaisha wananchi waliopo kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa. Katika kikao kazi hicho, Prof. Shemdoe na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Azania Bi. Esther Mangenya wamekubaliana kujenga mahusiano mazuri ili wananchi wanufaike na mchango wa Serikali na benki hiyo katika kuboresha miundombinu ya utoaji wa huduma za kijamii. Kwa kutambua mchango wa taasis...