Machapisho

USAFIRI WA SGR DAR ES SALAAM- DODOMA WAREJEA, TRC YAOMBA RADHI KWA USUMBUFU

Picha
  Na Hamida Ramadhani, Dodoma. SHIRIKA la reli Tanzania limeufahamisha umma wa Watanzania kuwa huduma za usafiri wa treni za SGR zimerejea na kuendelea kama kawaida, likiomba radhi kwa wateja wake kwa usumbufu uliojitokeza, shirika likiwashukuru pia Wananchi kwa uvumilivu wao katika kipindi ambacho huduma za usafiri huo zilipotatizika kutokana na hitilafu iliyotokea mapema leo Alhamisi Oktoba 23, 2025. Mapema leo Shirika la Reli Tanzania lilitoa taarifa kwa Vyombo vya habari likieleza kuhusu ajali ya Treni ya EMU iliyokuwa ikisafiri kutoka Dar Es Salaam kwenda Dodoma majira ya saa mbili asubuhi kutokana na hitilafu za uendeshaji, tukio ambalo lilitokea Kituo cha Ruvu na kwa taarifa za shirika hilo hakukuwa na athari kubwa za ajali hiyo. Timu ya wataalamu ikiongozwa na Katibu Mkuu wa uchukuzi, Mkurugenzi wa shirika la TRC, Vyombo vya ulinzi na usalama na menejimenti ya TRC ilianza haraka kushughulikia changamoto hiyo na kufanya uchunguzi wa kina wa kuhakikisha kuwa huduma hizo zimer...

DKT.ABBASI, MWAKILISHI MKAZI UNDP WAZINDUA UBORESHAJI MISITU NCHINI.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam. SERIKALI imezindua rasmi utekelezaji wa mradi mkubwa wa kimataifa wa mazingira ujulikanao kama “Mbinu Chanya na Jumuishi za Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi na Kulinda Bayoanuai” (Integrated Net-Zero Nature-Positive Solutions for Climate and Biodiversity Protection), unaolenga kuendeleza sekta ya misitu kwa lengo la kuinua maisha ya watu. Akizungumza leo Oktoba 23,2025 jijini Dar es Salaam wakati wa ufunguzi wa kikao cha kwanza cha Kamati ya Usimamizi wa Mradi huo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi, ambaye ni Mwenyekiti alisema mradi huo wenye thamani ya Dola za Marekani milioni 38 ni uthibitisho wa kuaminiwa kwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. “Mradi huu ni ushahidi wa juhudi za Serikali katika kulinda mazingira, kuhifadhi misitu na kuhamasisha nishati safi. Dunia inatambua uongozi wa Tanzania katika masuala ya uchumi wa kijani ndio maana baadhi ya wadau wa Mradi huu pamoja ...

TAARIFA KWA UMMA

Picha

REA YAENDELEA KUTEKELEZA KWA VITENDO MKAKATI WA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

Picha
Majiko banifu 4,836 kusambazwa na kuuzwa kwa bei ya ruzuku mkoa wa Njombe. Jiko moja kuuzwa kwa bei ya ruzuku ya TZS 8,850 tu,Kila walaya kupata majiko 1,209 Na Lunango Mleka, Njombe. MKUU wa  Wilaya ya Ludewa Mhe. Olivanus Thomas akimwakilisha Mkuu wa mkoa wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka leo Oktoba 20,2025 amezindua rasmi mradi wa usambazaji na uuzaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku mkoa wa Njombe. uzinduzi huo umeongozwa na mkuu wa wilaya , Maafisa kutoka REA pamoja na viongozi wengine wa mkoa, wilaya, kata, vijiji na vitongoji vyake.  Mhe. Olivanus amesema , lengo la uzinduzi  wa mradi huu ni kuutambulisha rasmi mradi kwa wananchi wa mkoa wa Njombe ambao ndio walengwa na wanufaika wa mradi. Mhe. Olivanus, amepongeza juhudi za Serikali na REA katika kufanikisha utekelezaji wa mradi na kuongeza kuwa lengo la Mkakati wa Nishati Safi ya Kupikia ni kuwa ifikapo mwaka 2034, asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia nishati safi ya kupikia, jambo ambalo litasaidia kutunza Afya...

DKT. MATARAGIO AAGIZA VIFAA VYOTE VYA UHAKIKI WA JOTOARDHI ZIWA NGOZI KUFIKA KWA WAKATI

Picha
  Ni baada ya kukagua mradi na kukuta baadhi ya vifaa bado havijafika Asisitiza mradi kukamilika kwa wakati ikiwa ni  utekelezaji wa Sera ya Nishati ya mwaka 2015 Kazi ya uhakiki wa Jotoardhi Ziwa Ngozi yafikia asilimia 60. Na Mwandishi Wetu, Mbeya. NAIBU Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Dkt. James Mataragio ameliagiza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Kampuni yake Tanzu ya Uendelezaji Jotoardhi (TGDC)  kuhakikisha kuwa vifaa vyote vya uhakiki wa rasilimali Jotoardhi  katika mradi wa Ziwa Ngozi  vinafika kwa wakati ili kazi za uhakiki  ziweze kumalizika kulingana na muda uliopangwa. Dkt. Mataragio ametoa maagizo hayo leo Oktoba 22, 2025 wakati wa ziara yake ya kukagua kazi zinazoendelea kutekelezwa katika mradi huo wilayani Rungwe mkoani Mbeya. “Huu mradi mnapaswa kuukamilisha kwa wakati kutokana na umuhimu wake nchini, tunapotekeleza miradi hii ya Jotoardhi tukumbuke kuwa tunatekeleza pia Sera ya Taifa ya Nishati ya Mwaka 2015 ambayo inasema Tanzania in...

WANAFUNZI WATAKIWA KUDUMISHA AMANI NA MSHIKAMANO

Picha
Na Mwandishi Wetu, Mara. AFISA Ushirikishwaji Jamii Mkoa wa Mara, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Thomas Mapuli, Oktoba 22,2025 amekutana na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mshikamano iliyopo katika Manispaa ya Musoma, ambapo ametoa elimu juu ya ukatili wa kijinsia na umuhimu wa kutunza amani katika jamii. Akizungumza na wanafunzi hao shuleni hapo ACP Mapuli aliwasisitiza vijana kuwa mabalozi wa amani na kuzingatia maadili mema, huku akiwataka kujiepusha na vitendo vya vurugu, ubaguzi, na ukatili wa aina yoyote, ikiwemo ule wa kijinsia. Aidha, aliwahimiza wanafunzi kuzingatia masomo yao na kuepuka vishawishi vinavyoweza kuhatarisha ndoto zao za baadaye, akibainisha kuwa elimu ndiyo ngao kuu ya kupambana na changamoto mbalimbali za kijamii na kiuchumi. “Jamii yenye amani huanza na mtu mmoja mmoja. Ninyi kama vijana mna wajibu wa kuwa mfano wa kuigwa, kujilinda na kuwalinda wengine dhidi ya ukatili wa kijinsia, na kushirikiana na vyombo vya dola kutoa taarifa za vitendo hivyo pindi vin...

SERIKALI KUPITIA UCSAF KUFIKISHA MAWASILIANO KATIKA MAENEO YA KIMKAKATI

Picha
Na Hamida Ramadhani, Dodoma. SERIKALI kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) inatarajia kuanza utekelezaji wa awamu mpya ya ujenzi wa minara 280 ya mawasiliano, ambapo baadhi ya minara hiyo itajengwa katika maeneo ya mipakani, mbuga za wanyama, na njia kuu za reli za SGR na TAZARA. Hatua hii inalenga kuhakikisha huduma za mawasiliano zinapatikana katika maeneo yote yenye umuhimu wa kimkakati kwa usalama, utalii na maendeleo ya Taifa. Mtendaji Mkuu wa UCSAF, Mhandisi Peter Mwasalyanda, amesema utekelezaji wa awamu hiyo mpya unafuatia mafanikio makubwa ya mradi wa awali wa minara 758, ambao umefikia zaidi ya asilimia 98 ya utekelezaji. Ameeleza kuwa kukamilika kwa mradi huo kumechangia kupunguza kwa kiasi kikubwa pengo la mawasiliano katika maeneo ya vijijini na pembezoni. Jumla ya vijiji 1,407 ambavyo awali havikuwa na mawasiliano, sasa vinafikishiwa huduma hiyo muhimu, hatua inayoboresha maisha ya wananchi na kuongeza fursa za kiuchumi. Aidha, Mhandisi Mwasalyanda ameongeza kuwa...

WAFCON QUALIFIERS 2026

Picha
23’ Tanzania 🇹🇿 1️⃣-0️⃣ 🇪🇹 Ethiopia  ⚽️Aisha Mnunka  @twigastars_ @caf_online

WANAWAKE WA TEMEKE WAANZA SHAMRASHAMRA ZA KUMPOKEA MGOMBEA WA URAIS DKT. SAMIA

Picha
Na Hamida Ramadhani, Dar es Salaam. MWENYEKITI wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi Tanzania (UWT) Ndg. Mary Pius Chatanda (MCC) ambaye pia ni Mratibu wa Kampeni za CCM Jijini DSM, Leo tarehe 19 Oktoba, 2025, apokelewa na matembezi ya Wanachama wa UWT Wilaya ya Temeke yaliyoambatana na Ngoma kuelekea kwenye Ukumbi wa Taifa Pub, Kata ya Mibulani, kwa lengo la kufanya Kikao na wajumbe wa Baraza la UWT Wilaya ya Temeke, ili kujiweka sawa na Mapokezi ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mgombe Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), katika kufanya Mikutano ya Kampeni ndani ya Jiji la DSM, na kunadi ilani ya CCM 2025/2030 na kuomba kura za ndiyo kwa Wananchi kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025.   (