Machapisho

JESHI LA POLISI LATAKIWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA WADAU WA UCHAGUZI NCHINI.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Moshi.  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema ni muhimu Jeshi la Polisi kuimarisha ushirikiano wa karibu na wadau wote wa uchaguzi, hatua ambayo itasaidia kuhakikisha kila mdau anatendewa haki, na kuondoa tofauti zinazoweza kusababisha migongano.   Makamu wa Rais ametoa wito huo wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi unaofanyika katika ukumbi wa Chuo Cha Polisi (CCP) Moshi Mkoani Kilimanjaro. Amesema Baadhi ya maeneo muhimu ya ushirikiano ni pamoja na kuhakikisha mikutano ya kampeni inafanyika kwenye maeneo yaliyoruhusiwa na ndani ya muda uliopangwa,  Kuzuia maandamano yasiyo na kibali, kuimarisha ulinzi wa wagombea na viongozi wa vyama vya kisiasa, bila kujali vyama vyao au itikadi zao pamoja na kudhibiti misongamano mikubwa ya watu ili kuhakikisha shughuli nyingine za kijamii na kiuchumi zinaendelea bila usumbufu.   Pia Makamu wa Rais amelitaka Jeshi la Polisi ku...

RAIS MWINYI ATEMBELEA ENEO LA OFISI ZA MJI WA SERIKALI NA LINALOJENGWA UWANJA MPYA WA AFCON

Picha
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar.  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameeleza kuwa Serikali inaendelea kusimamia utekelezaji wa mradi mkubwa wa uwanja wa AFCON pamoja na miundombinu mbalimbali inayojengwa Fumba, hivyo ni muhimu kubaini mapema maeneo yatakayotumika kwa mradi huo ili kuepusha mwingiliano wa matumizi ya ardhi katika eneo hilo kati ya taasisi husika. Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 11 Agosti 2025, katika kikao maalum na mawaziri mbalimbali akiwemo Mhe. Rahma Kassim Ali, Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi, Mhe. Shariff Ali Shariff, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji, Mhe. Tabia Maulid Mwita, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mhe. Dkt. Khalid Salum Mohamed, Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, pamoja na Taasisi ya Ofisi ya Rais, Ufuatiliaji na Usimamizi wa Utendaji Serikalini (ZPDB), kwa lengo la kupata uelewa wa pamoja kuhusu matumizi sahihi ya ardhi katika maeneo ya uweke...

MADEREVA, ABIRIA WAPATIWA ELIMU YA USALAMA BARABARANI NA MATUMIZI SAHIHI YA VYOMBO VYA KUZIMIA MOTO IGUNGA.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Igunga.  MADEREVA na Abiria katika Kituo cha Mabasi Wilaya ya Igunga Mkoani Tabora wamepatiwa Elimu ya Usalama Barabarani na Mabalozi wa Usalama Barabarani Wilaya ya Igunga (RSA) yenye lengo la kuendelea kuwakumbusha Madereva na Abiria kufuata sheria za usalama barabarani ili kunguza ajali zitokanazo na ubovu wa magari na uzembe wa Madereva.  Elimu hiyo imetolewa na Shirika lisilo la Kiserikali la Road Safety Ambassadors (RSA) kwa kushirikiani na Jeshi la Polisi kitengo cha Usalama Barabarani na Jeshi la Zimamoto wilaya ya Igunga ambapo wametoa Elimu ya Usalama Barabarani, Wajibu na Haki za Abiria, Elimu ya tahadhari  ya majanga ya Moto pia imbeambatana na zoezi la ukaguzi wa magari, vifaa vya kuzimia moto na ukaguzi wa leseni kwa madereva.  Akitoa Elimu ya tahadhari ya majanga ya moto Koplo Shadrack Mweya kutoka Jeshi la Zimamoto amewataka madereva kuhakikisha magari yao yanakuwa na vifaa vya kuzimia moto ambavyo havijaisha muda wa matumizi, milan...

RAIS MWINYI:SMZ ITAENDELEA KUIMARISHA MIUNDOMBINU YA USAJILI KIDIJITALI.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar.  RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema kuwa Serikali itaendelea kuimarisha miundombinu ya usajili kidijitali wa matukio ya kijamii kutokana na umuhimu wake kwa maendeleo ya nchi. Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 10 Agosti,  2025 katika kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Usajili Barani Afrika yaliyofanyika katika Ukumbi wa Idrissa Abdulwakil, Kikwajuni, Mkoa wa Mjini Magharibi. Ameeleza kuwa hatua hiyo itaongeza ufanisi na utoaji wa huduma bora kwa wananchi unaofanywa na Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii Zanzibar (ZCSRA) katika usajili wa vizazi, vifo, talaka, ndoa na vitambulisho vya Mzanzibari Mkaazi. Rais Dkt. Mwinyi amesema hakuna maendeleo ya kweli bila usajili wa utambulisho wa wananchi katika mifumo imara inayotambulika kisheria na inayotumia teknolojia ya kisasa ya kidijitali. Aidha, Dkt. Mwinyi ametoa rai kwa ZCSRA kuanzisha kampeni maalum kwa kushirikiana na masheha kuha...

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI.

Picha

MWILI WA SPIKA MSTAAFU WA BUNGE LA TANZANIA NA ALIYEKUWA MBUNGE WA KWONGWA UMEWASILI VIWANJA VYA BUNGE.

Picha
MWILI wa hayati Spika Mstaafu wa Bunge na aliyekuwa Mbunge wa Kongwa  Mhe. Job Justino Ndugai, umeshawasili katika viwanja vya Bunge Jijini Dodoma kwa ajili ya viongozi wa kitaifa, familia, wabunge na wananchi kutoa heshima zao za mwisho na baada ya hapo mwili wa hayati Job Yustino Ndugai utaelekea nyumbani kwake Kongwa Jijini Dodoma.

UJENZI WA JENGO LA UBIA KATI YA NHC NA TOSH LOGISTICS KARIAKOO.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Kariakoo- Dar es Salaam.  SHIRIKA la Nyumba la Taifa (NHC) kwa ubia na Tosh Logistics Ltd linaendelea na ujenzi wa jengo la kisasa la biashara na makazi katika eneo la Tandamti, Kariakoo – Dar es Salaam. Mradi huu unaojengwa kwenye viwanja sita (3/16 hadi 14/16) unalenga kubadilisha sura ya Kariakoo kwa kujenga majengo ya kisasa yenye matumizi mchanganyiko. Jengo limegawanywa katika Block A na Block B ambapo kazi zinasonga mbele kwa kasi, block A ipo hatua ya ujenzi wa ghorofa ya pili, block B imefikia ghorofa ya sita. Mradi huu unatekelezwa kuanzia Oktoba 15, 2024 hadi Oktoba 15, 2026, ni sehemu ya jitihada za NHC kukuza miundombinu ya kisasa na kuchochea uwekezaji kwenye maeneo ya mijini kupitia ubia wa kimkakati na sekta binafsi. #NHCProjects #ToshLogistics #MajengoYaKisasa #KariakooMpya #UjenziEndelelevu #PublicPrivatePartnership #MaishaNiNyumba#CrownMedia #Ayotv

MATUKIO KATIKA PICHA.

Picha
MGOMBE wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya ACT Wazalendo Ndugu Luhaga Mpina, Mgombea Mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndugu Fatma Ferej na Mgombea wa Urais wa Zanzibar Ndugu Othman Masoud Othman wamepokelewa na maelfu ya wanachama wa ACT Wazalendo na wananchi wa Zanzibar kwa ajili ya kujitambulisha upande wa Unguja leo tarehe 9 Agosti 2025. Oktoba #LindaKura #MuhuniHasusiwi @ACTwazalendo