NENDENI MKAWASILIZE WANANCHI WA SONGWE- CHATANDA
Na Hamida Ramadhani, Songwe.
MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake Tanzania Taifa (UWT), Ndg. Mary Pius Chatanda (MCC), ametoa wito kwa Wagombea wa Ubunge na Udiwani kuhakikisha wanatimiza dhamira zao za kuwatumikia wananchi mara baada ya kuteuliwa na kuaminiwa na Chama cha Mapinduzi (CCM)
Akizungumza katika Mkutano wa Hadhara leo, uliofanyika Kata ya Msangano, Jimbo la Mombo, mkoani Songwe, Chatanda amesisitiza kuwa Wananchi wanahitaji kusikilizwa, kutembelewa na kuungwa mkono katika kutatua changamoto zao na kuinua Maendeleo katika maeneo yao.




Maoni