Machapisho

WANANCHI WAHIMIZWA KUTUMIA LANDMAX KUEPUKA UTAPELI WA ARDHI

Picha
   Na Hamida Ramadhan,Dodoma MBUNGE wa Jimbo la Mbozi, Onesmo Mnkondya, amewataka wananchi na madalali wanaohusika na biashara ya ardhi kutumia huduma za Landmax Real Estate Company Limited ili kufanya uwekezaji kwa usalama na kuondokana na migogoro inayotokana na mauzo au ununuzi usio rasmi wa ardhi. Mnkondya, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Landmax Real Estate Company Limited, amesema hayo Juni 24, 2026 jijini Dodoma wakati wa hafla ya uzinduzi wa ofisi za kampuni hiyo. Amesema Landmax imeanzishwa kwa lengo la kuwasaidia wananchi kupata ardhi salama na makazi bora huku ikichangia kupunguza migogoro ya ardhi. Aidha, amebainisha kuwa kampuni hiyo inatoa huduma mbalimbali ikiwemo uuzaji na ununuzi wa ardhi na mali isiyohamishika, ushauri wa uwekezaji wa ardhi, usimamizi wa mali, urasimishaji wa nyaraka za ardhi, uendelezaji wa miradi, tafiti za soko pamoja na ushirikiano katika miradi ya maendeleo. “Tunawaalika wananchi na madalali wote wanaotaka kununua au kuuza ardhi kufika ofisi...

RC MTANDA AWATAKA MISUNGWI DC KUSHIRIKIANA KUWALETEA MAENDELEO WANANCHI

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Mwanza.  MKUU wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameitaka halmashauri ya wilaya ya Misungwi kuimarisha umoja baina ya Baraza la Madiwani na Menejimenti kuwaletea wananchi huduma bora za kijamii kwa kutumia mapato ya ndani kwa kujenga shule, vituo vya afya na miundombinu ya maji. Mhe. Mtanda amefikia hatua ya kutoa agizo hilo baada ya kubaini uwajibikaji duni kwenye ukusanyaji kwa mwenendo wa miaka mitatu na udhaifu kwenye kujibu hoja ambapo kwa mwaka husika wa fedha hoja 81 zimetekelezwa 23 pekee sawa na asilimia 28.4 huku hoja 57 bado hazijajobiwa sawa na asilimia 70.4. Ametoa agizo hilo leo tarehe 24 juni, 2026 wakati akihutubia Mkutano Maalumu wa Baraza la Madiwani wa kujadili hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) pamoja na Maagizo ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (LAAC) 2024/25 ambapo wamepata hati safi. "Maendeleo ya Misungwi yanawategemea ninyi viongozi na watendaji mlioaminiwa hapa, mkileta mzaha kwenye uwaji...

RC MTANDA AIAGIZA KWIMBA DC KUTUMIA MAPATO YA NDANI KWA MIRADI YA KIMKAKATI

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Mwanza.  MKUU wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewapongeza Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba kwa kufikia malengo kwenye ukusanyaji wa mapato kwa kipindi cha miaka minne mfululizo ambapo amewataka kutumia mapato hayo kujenga miradi mikubwa ya kimkakati. Ametoa agizo hilo leo tarehe 24 juni, 2026 wakati akihutubia Mkutano Maalumu wa Baraza la Madiwani wa kujadili hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) pamoja na Maagizo ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (LAAC) 2024/25 ambapo wamepata hati safi. Mhe. Mtanda amesema ni wakati sasa kwa halmashauri kuwekeza kwenye miradi mikubwa ambayo italeta makusanyo makubwa zaidi na kuongeza wigo wa ukusanyaji mapato badala ya kujenga miradi mingi midogo pekee ambayo kimsingi haitumiki kurejesha fedha. "Tumieni asilimia 40 ya makusanyo yenu kwa mujibu wa sheria kufanya hata mradi mmoja mkubwa ambao utakuwa alama kama wa uwanja wa mpira ambao mtajihakikishia ukusanyaji wa mapato kwa siku...

DG TASAC: KUKAMILIKA KWA MV LIEMBA KUTAIMARISHA BIASHARA, USAFIRI NA UCHUMI KIGOMA

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Kigoma.  MKURUGENZI Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), Bw. Mohamed Salum, amesema kukamilika kwa ukarabati wa meli ya MV Liemba kutaimarisha huduma za usafiri wa majini, kuchochea biashara na kuharakisha maendeleo ya uchumi wa Mkoa wa Kigoma na ukanda mzima wa Ziwa Tanganyika. Bw. Salum amesema hayo leo, tarehe 23 Juni, 2026 alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ukarabati wa meli hiyo katika Bandari ya Kigoma, ikiwa ni sehemu ya shughuli za Maadhimisho ya 16 ya Siku ya Mabaharia Duniani yanayoendelea mkoani humo. Amesema wananchi wanaoishi katika maeneo yanayozunguka Ziwa Tanganyika wanategemea kwa kiwango kikubwa usafiri wa majini kwa shughuli za biashara, usafirishaji wa bidhaa na huduma za kijamii, hivyo kukamilika kwa MV Liemba kutaboresha huduma hizo na kuongeza ufanisi wa usafiri salama na wa uhakika. "MV Liemba ni meli yenye umuhimu mkubwa kwa wananchi wa ukanda wa Ziwa Tanganyika. Kukamilika kwake kutaimarisha usafiri salama, k...

RC MTANDA: ONGEZENI MAPATO, FUTENI HOJA ZA CAG

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Mwanza.  MKUU wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameutaka Uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema kuongeza juhudi katika ukusanyaji wa mapato ya ndani ili kuimarisha utoaji wa huduma na kuhakikisha halmashauri inapata uwezo wa kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi. Mhe. Mtanda ametoa kauli hiyo wakati akizungumza katika Mkutano wa Baraza Maalumu la kujadili hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), amesisitiza kuwa mapato ndiyo msingi wa uendeshaji wa halmashauri na huwezesha watumishi na madiwani kupata stahiki zao kwa wakati. Aidha, ameutaka Uongozi wa Halmashauri kusimamia kikamilifu miradi ya maendeleo ili kuhakikisha thamani ya fedha inaonekana na wananchi wanapata manufaa yaliyokusudiwa kupitia miradi inayotekelezwa katika maeneo yao. Kuhusu maagizo ya Kamati za Bunge, RC Mtanda amesema Halmashauri inapaswa kuandaa taarifa za kina kuhusu utekelezaji wa maelekezo hayo badala ya kutoa taarifa za jumla zisizoonyesha hatua zilizo...

RC MTANDA AKABIDHI PIKIPIKI 18 KWA VIKUNDI 2 VYA VIJANA BUCHOSA

Picha
Na Mwandishi Wetu, Mwanza.  MKUU wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo tarehe 23 Juni, 2026 amekabidhi pikipiki 18 zenye thamani ya Tshs. Milioni 54.9 vya vikundi viwili vya vijana vya Bodaboda Lugasa na Waungwana Group Mbugani. Akiongea kwenye hafla ya makabidhiano hayo Mhe. Mtanda ameipongeza halmashauri hiyo kwa kuendelea kufanya vizuri kwenye eneo la matumizi ya fedha za mapato ya ndani kwa maendeleo ya wananchi. Halmashauri ya Buchosa inafanya vizuri sana , kwanza kwenye kukusanya mapato na pili kwenye kutumia kwa ajili ya maendeleo ya wananchi kwa kutumia mapato yao kununua vyombo kama pikipiki na kukopesha kwa vijana. Amesema Mkuu wa Mkoa. Aidha, ametoa wito kwa halmashauri hiyo kusimamia urejeshaji wa mikopo hiyo ili itumike kununua zingine na kuwezesha makundi mengine yaweze kukopeshwa. Aidha, amewataka vijana walionufailka na mkopo huo kuheshimu sheria za usalama barabarani kwa kuendesha kwa staha kwa usalama wao na wa watumia barabara wengine aidha kuzitumia pia kwa mal...