KAPINGA, LONDO WAANZA SAFARI YA KUIMARISHA SEKTA YA VIWANDA NA BIASHARA
Na Mwandishi Wetu, Dodoma. WAZIRI wa Viwanda na Biashara Mhe. Judith Kapinga (Mb), ameongoza watumishi wa Wizara hiyo kumpokea Naibu Waziri mpya, Mhe. Denis Londo (Mb), huku akisisitiza umuhimu wa ushirikiano wa karibu katika kutekeleza majukumu ya wizara kwa maslahi mapana ya Taifa. Akizungumza Januari 15, 2026 katika Ofisi za Wizara hiyo jijini Dodoma, Mhe. Kapinga ameahidi kumpa ushirikiano wa kutosha Naibu Waziri Londo na kuelekeza Menejimenti pamoja na Watumishi wa Wizara kushirikiana kwa karibu ili kufanikisha malengo waliyojiwekea katika kuendeleza sekta ya viwanda na biashara nchini. “Ninawahimiza Menejimenti na watumishi wote kushirikiana kikamilifu na Naibu Waziri ili kwa pamoja tuweze kutimiza majukumu yetu kwa ufanisi na kufikia malengo ya Wizara kwa maslahi ya Taifa,” amesema Mhe. Kapinga. Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Denis Londo (Mb), amesema kazi iliyo mbele yao ni kubwa na kwamba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Sulu...